JavaScriptSDK

Saturday, February 11, 2017

MPANGO WA KUJITOLEA DAMU WAFANA, ALHAMDULILLAH

Kulia: Qaid Ilaqa ya Dar es salaam
Kushoto: Sadr Majlis Khuddamul Ahmadiyya Tanzania
Kwa fadhila za Allah, Majlis Khuddamul Ahmadiyya Ilaqa ya Dar es salaam wamefanikisha tukio la uchangiaji damu lililofanyika katika Ofisi za Damu Salama kanda ya Mashariki kama lilivyotangazwa hapo kabla.

Muhtamim Tarbiyyat katika mchakato wa kutoa damu
Toka Kulia: Qaid Ilaqa, Muhtamim Maal na
Muhtamim Khidmat Khalq katika mchakato wa kutoa damu
Tukio hilo lilihudhuriwa na Khuddam wapatao ishirini na nne (24), akiwemo na Sadr Majlis pamoja na baadhi ya wana Majlis Mulk pia.

Tukio hilo liliambatana na kikao pamoja na uongozi wa Damu Salama kanda ya Mashariki kilichokuwa na madhumuni ya Kufahamiana zaidi na kuzijadili changamoto za pande zote katika Masuala yote yahusuyo damu.









Kabla ya zoezi la utoaji damu kuanzishwa rasmi, washiriki waote walipata maelekezo ya mazingira na Kufahamishwa shughuli za idara kadhaa zilizopo hapo.

 







#KhidmatKhalq        @ChangiaDamuTZ    #GiveBlood     #BelieveInGiving   #OkoaMaisha

No comments: