JavaScriptSDK

Tuesday, May 31, 2016

TAIFA HALIWEZI KUIMARIKA PASIPO VIJANA KUWA IMARA!



Khuddam-ul Ahmadiyya ni Tanzimu au Tawi la Vijana wa Kiislamu wa Jumuiya ya Waislamu Wa-Ahmadiyya Duniani. Tanzimu au Tawi hili ni la vijana wa Kiahmadiyya kuanzia miaka 15 mpaka 40. Khuddam-ul Ahmadiyya ilianzishwa rasmi na Khalifatul Masih II, Hadhrat Mirza Bashiruddin Mahmood Ahmad (ra) mwaka 1938. Kulingana na Khalifatul Masih II, maneno Khuddamul Ahmadiyya maana yake vijana waliopo katika kundi hili ni Watumishi wa Ahmadiyya. Katika hotuba yake yenye kukumbukwa sana aliyoitoa Aprili 1, 1938,  katika msikiti wa Al Aqsa uliopo Qadian, India, Khalifatul Masih II (ra):
http://www.amjinternational.org/wp-content/themes/striking/cache/images/KM2-212x300-212x300.jpg
Khalifatul Masih II(ra), Mwanzilishi wa Majlis Khuddamul Ahmadiyya
“Nimekuwa nikisisitiza jumuiya kuhusiana na ukweli kwamba, Kuimarika kwa Taifa Lolote Hakuwezi Kutimia Pasipo Vijana Wake Kuwa Imara.Jumuiya yetu haiwezi kupata maenedeleo ya kweli mpaka pale vizazi vipya havijatekeleza Ujumbe na Mafundisho sahihi Kiislamu ambayo Mtume S.A.W aliyaleta Duniani. Khuddamul Ahmadiyya maana yake ni Watumishi wa Ahmadiyya. Jina hili daima litaendelea kuwakumbusha kwamba wao ni watumishi, na si kutumikiwa. Mnatakiwa  mdhihirishe na muimarishe vipawa vyenu kwamna iliyo bora. Ikiwa mtaonesha mfano mwema kwa wengine, itakuwa rahisi kuwavutia kujiunga na jumuiya yenu.”

https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/9/98/Khuddam-ul-Ahmadiyya_1-2.svg/2000px-Khuddam-ul-Ahmadiyya_1-2.svg.png
Bendera rasmi ya Majlis Khuddamul Ahmadiyya ambayo inatumiwa na vijana wa Ki-Ahmadiyya kuanzia miaka 15 hadi 40
Majlis Khuddamul Ahmadiyya Tanzania ni sehemu ya kauli hiyo ya Khalifatul Masih II (ra) kwani madhumuni ya kuanzishwa kwake yanabeba maana nzima ya Utumishi si kwa Jumuiya pekee bali utumishi kwa viumbe vyote vya Allah kwa lengo la kupata radhi yake.

ITAENDELEA…

Wednesday, May 25, 2016

UAHMADIYYA SI DINI MPYA


https://ziahshah.files.wordpress.com/2010/09/huzur-ii1.jpg
Hadhrat MIRZA MASROOR AHMAD (a.t.b.a), Kiongozi wa Kiroho wa Jumuiya Ya Waislamu Waahmadiyya Duniani


Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema,

Mwingi wa Ukarimu.



Makala ifuatayo ina maelezo ya itikadi na mafundisho ya Jumuiya ya Waisalmu Ahmadiyya katika Uislamu, kifafanuzi cha madai ya Mwanzilishi wake Mtakatifu na hoja za msingi wa madai yake. Makusudio yangu katika kuandika makala haya , msomaji mpenzi, ni kukufikishia wewe na wengine, Ujumbe ambao Mwenyezi Mungu Ameuleta kwa wanadamu siku hizi ili kuwakusanya kwenye Uislamu na Mtume Wake Mtakatifu (s.a.w.). Kama uchukue taabu ya kuzisoma kurasa hizo zote, sio tu kwamba utapata shukurani zangu nyingi, bali vilevile utajipatia radhi ya Mwenyezi Mungu.



                                                 UAHMADIYYA SI DINI MPYA



Kwanza ningependa kubainisha suala moja kwamba majina Mwahmadiyya, Uahmadiyya n.k., hayaashirii kwenye dini mpya. Waahmadiyya ni Waislamu na dini yao ni Islam. Kuutoka Uislamu hatua moja tu wanaamini kuwa ni haramu na kukosa bahati. Naam, Waahmadiyya wametwaa majina, Uahmadiyya, Mwendeleo wa Ahmadiyya na kadhalika. Lakini kutwaa jina sio maana yake kuwa ni dini mpya. Majina Mwahmadiyya, Uahmadiyya n.k., yanakusudiwa tu kuwapambanua Waislamu Waahmadiyya na Waislamu wengine.



                                                  UISLAMU ULITABIRIWA



Jina Islam, ni jina zuri ambalo Mwenyezi Mungu mwenyewe amewapa wafuasi wa Mtukufu Mtume s.a.w. na ambalo miaka mingi kabla yake lilipata nafasi ya heshima katika bishara za Manabii wa zamani. Quran Tukufu inasema:



"Yeye aliwaiteni Waislamu tangu zamani na katika (Quran) hii pia"

(22:79).

Na katika Biblia imeandikwa:

"Nawe utaitwa jina jipya litakalotajwa kwa kinywa cha Bwana" .(Isaya 62:2).

Hakuna jina jingine linaloweza kuwa na baraka zaidi na takatifu kuliko lile ambalo Mwenyezi Mungu amelivisha heshima kwa kuwafanya Manabii wengine walitabiri. Nani ataliacha jina hili? Jina hili ni penzi kwetu kuliko maisha yetu. Na dini inayoungana na jina hili ndicho chanzo cha pekee cha uhai wa kiroho. Lakini kama ilivyo katika wakati wetu huu, firka (makundi) mbalimbali za Waislamu, kwa sababu ya hitilafu ya itikadi zao na mwendo, wamejitwalia majina mbalimbali, imetuwia lazima nasi pia tuwe na jina maalum ili tujipambanuwe katika Waislamu wengine. Jina bora tuliloweza kutwaa ni jina Mwahmadiyya au Uahmadiyya. Jina hili linalingana na wakati huu. Huu ndio wakati ulioteuliwa kwa ajili ya kutangazwa dunia nzima ule Ujumbe wa Kiulimwengu wa Mtukufu Mtume s.a.w. Ndio wakati wa kuenezwa sifa za Mwenyezi Mungu na kuenezwa Elimu ya Fadhili na Uzuri Wake, ndio wakati wa kudhihirishwa sifa ya Ahmadiyyat baada ya kudhihirishwa sifa ya Muhammadiyyat. Hakuna jina zuri lenye kutambulisha siku hizi zaidi ya hili tuliloweza kutwaa. Tu Waislamu kwa moyo na roho. Tunashika itikadi ambazo Mwislamu wa kweli inamlazimu kuzishika na tunakana itikadi ambazo Mwislamu wa kweli inamlazimu kuzikana. Kama licha ya kushiriki kwetu kwa moyo kwenye kweli za Uislamu na kufuata kwetu amri za Mwenyezi Mungu, mtu yeyote atupe sifa ya ukafiri na atueleze kama waghushi au waaminio wa dini mpya, ni mtu katili sana. Atahukumiwa na Mwenyezi Mungu. Mtu anaweza kulaumiwa kwa yale anayoyatangaza kwa mdomo wake, sio kwa yale yaliyo moyoni mwake. Kwani, nani awezaye kusema yaliyomo moyoni mwa mwingine? Kama mtu anamshutumu mwenzake kwa kusema jambo moja na kuamini jingine, anajiinua mwenyewe kwenye cheo cha Mwenyezi Mungu. Ni Mwenyezi Mungu tu ndiye ajuaye yaliyomo mioyoni mwa watu. Yeye peke yake anaweza kusema yale afikiriayo mtu na yale anayoamini. Mtukufu Mtume s.a.w. anakubali ukomo huu wa kibinadamu. Na tena ni nani angeweza kujua moyo wa mtu zaidi kuliko yeye? Anasema juu yake mwenyewe:



"Miongoni mwenu kuna wanaoniletea mabishano yao. Mimi ni mtu

kama ninyi. Inawezekana baadhi yenu wakawa watetezi hodari

kuliko wengine. Hivyo, kama nikimpa mmoja haki ya mwingine,

nitakuwa ninampa sehemu ya moto. Ni juu yake kukataa."

(Sahihi

Bukhari, Kitabul-Ah'kaam Babu Mauizatul-Imam lilikhusuum).



Tunasoma katika Hadithi kwamba Usama bin Zaid aliteuliwa na Mtukufu Mtume s.a.w. kuwa Amir wa kikosi fulani. Usama alipambana na kafiri mmoja na kumshambulia. Kafiri huyu alipokaribia kuuawa, alitamka Kalima, akithibitisha kuamini ukweli wa Dini ya Islam. Hata hivyo Usama alimwua. Mtukufu Mtume s.a.w. kusikia hivi, akamkaripia Usama. Akijitetea Usama alisema:

"Oo Mtume wa Mwenyezi Mungu, alifanya vile kwa woga."

Mtukufu Mtume s.a.w. akamjibu, "Kwa nini? Je, ulipasua moyo

wake ukauona? (Masnud, Imam Ahmad bin Hambal).



Elimu ya yale yapitayo mioyoni mwa watu haikupewa wanadamu. Haikumpasa Usama kudhani kama Kalima aliyotamka mtu huyu ilikuwa ni matokeo ya woga au la. Kwahiyo, tunaweza kulaumiwa kwa yale tuyatamkayo, sio kwa yale yanayoweza kudhaniwa kuwa yamo mioyoni mwetu. Yaliyomo mioyoni mwetu anayajua Mwenyezi Mungu tu. Anayedai kumlaumu mwenzake kwa yaliyomo moyoni mwake ni mwongo. Yeye anakiuka mipaka yake na atahukumiwa na Mwenyezi Mungu. Hivyo, sisi wa Jumuiya ya Ahmadiyya tunapotangaza kuwa tu Waislamu, hapana mwenye haki kusema kwamba Uislamu wetu ni wa kujisingizia; ya kwamba mioyoni tunakana Uislamu au tunamkana Mtume Mtukufu s.a.w.; na ya kwamba tuna Kalima mpya au kuelekea Kibla kipya tunaposali. Kama inaweza kuwa haki kwa wengine kutupa sifa hizi, basi inaweza kuwa haki kwetu kutoa sifa hizi kwa watu wengine. Tungeweza kusema kuwa tangazo lao la Uislamu ni kisingizio, kwamba Mungu apishe mbali, wanaukana Uislamu na kumtukana Mtukufu Mtume s.a.w. wanaporudi majumbani kwao. Lakini hatuwezi kupotezwa na upinzani. Hatutasema juu ya yeyote kwamba anasema jambo moja na kuamini jingine; ya kwamba ana jambo moja midomoni mwake na jingine moyoni mwake. Kwa amri ya Sheria, uamuzi wetu juu ya wengine utafuata yale waliyonayo na wanayoyatangaza waziwazi.

https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/9/91/Hazrat_Mirza_Nasir_Ahmad_Mash_III_(1967).jpg
HADHRAT MIRZA NASIRUDDIN AHMAD (RA) KHALIFATUL MASIH III


ITIKADI ZA WAAHMADIYYA



Sasa ninaendelea kueleza itikadi zinazoshikwa na Jumuiya yetu ili uone kama kuna yoyote iliyo kinyume na Uislamu:-



(1) Tunaamini kwamba Mwenyezi Mungu yupo; kushiriki katikakuamini kuwapo Kwake ni kutangaza ukweli wa maana sana; sio kufuata mawazo au dhana.



(2) Tunaamini kwamba Mwenyezi Mungu ni Mmoja. Hana mshirika hapa wala mbinguni. Kila kitu kingine ni kiumbe Chake na kinategemea msaada Wake. Hana mwana wala binti. Hana baba wala mama. Hana mke wala ndugu. Ni wa pekee katika Umoja Wake na katika Nafsi Yake.



(3) Tunaamini kwamba Mwenyezi Mungu ni Mtakatifu, ameepukana na kila upungufu na ni mwenye kila ukamilifu. Hakuna upungufu unaoweza kuonekana ndani Yake, na hakuna ukamilifu usioweza kupatikana ndani Yake. Uwezo Wake hauna ukomo. Na ndivyo ilivyo Elimu Yake. Amekizunguka kila kitu na hakuna kinachomzunguka Yeye. Ni wa Mwanzo na wa Mwisho, Yu Dhahiri na Amejificha pia. Ndiye Mwumbaji na Mola wa viumbe vyote. Utawala Wake haujapata kushindwa, haushindwi, na hautashindwa kamwe. Ameepukana na kufa. Ni Mwenye uhai wa milele. Hapati upungufu wowote. Matendo yake ni ya hiyari Yake, halazimishwi. Anautawala ulimwengu wote hivi sasa kama alivyokuwa akiutawala zamani. Sifa Zake ni za milele, Uwezo Wake u dhahiri siku zote.



(4) Tunaamini kwamba Malaika ni sehemu ya viumbe vya Mwenyezi Mungu. Wanafuata kanuni iliyoelezwa na Quran Tukufu:



                                     "Wanafanya wanayoamrishwa" (16:51).



Kwa Hekima Yake wameumbwa ili wafanye kazi fulani fulani maalum. Kuwapo kwao ni hakika na kutajwa kwao ndani ya Kitabu Kitakatifu si kwa methali. Wanamtegemea Mwenyezi Mungu kama wamtegemeavyo wanadamu au viumbe Vyake vingine. Hawategemei wao kwa kudhihirisha Uwezo Wake. Laiti Angetaka, Angeumba ulimwengu bila Malaika, lakini Hekima Yake kamilifu ilitaka kuumbwa kwao. Kwa hivi Malaika wakawapo. Mwenyezi Mungu aliumba nuru kwa ajili ya macho na mkate kwa ajili ya njaa. Aliumba nuru na mkate siyo kwa sababu alikuwa na haja navyo, la; kadhalika Hakuwaumba Malaika kwa sababu Anawategemea, bali Malaika wanadhihirishatu matakwa na Hekima ya Mwenyezi Mungu.

(5) Tunaamini kwamba Mwenyezi Mungu Anasema na watumishi Wake wateule na kuwafunulia makusudio Yake. Ufunuo wa Mungu hushuka kwa maneno. Mpokeaji wa ufunuo hatoi maana wala maneno ya ufunuo. Vyote hutoka kwa Mwenyezi Mungu. Ufunuo unatoa haja hasa ya mtu. Mtu anaishi kwa huo na kwa njia ya huo mtu anapata kuungana na Mwenyezi Mungu. Maneno ya ufunuo ni ya pekee katika nguvu na utukufu. Hakuna mtu awezaye kuyatunga maneno hayo. Yanabeba hazina ya elimu na hekima. Yako kama mgodi ambao unakunufaisha zaidi ukiendelea kuchimba. Kwa kweli, mgodi si kitu mbele ya ufunuo. Mgodi unaweza kwisha, lakini sio hekima ya ufunuo. Ufunuo uko kama bahari yenye ambary kwa juu yake na chini yake kuna lulu za thamani sana. Wale wanaoelekea bahari wanaburudishwa na manukato, na wale wanaozama wanakuta lulu chini yake. Ufunuo ni wa namna nyingi. Baadhi ya wakati unaleta amri na Sheria, pengine maonyo na mawaidha. Baadhi ya wakati unaleta elimu ya ghaibu, pengine hazina za elimu za kiroho. Baadhi ya wakati unaleta furaha na radhi ya Mwenyezi Mungu, pengine wajulisha makasiriko Yake, pengine wadhihirisha mapenzi Yake, na pengine humwelekeza mtu kwenye wajibu wake kwa kumkaripia . Baadhi ya wakati unafundisha tabia njema za ndani na pengine unaleta elimu Yake juu ya mwendo mbaya uliojificha wa mtu. Kwa ufupi, itikadi yetu ni kwambaMwenyezi Mungu anaeleza matakwa Yake kwa watumishi Wake. Maneno haya ni mbalimbali kwa watu wa vyeo na hali mbalimbali na huwa ya namna nyingi. Katika maneno yote ya Kiungu, yaliyokamilika zaidi na bora zaidi ni maneno ya Quran Tukufu. Sheria iliyoelezwa na Quran Tukufu na mwongozo wa kiroho uliomo ndani yake ni wa milele. Hautabatilishwa na ufunuo wowote

mwingine wa Mwenyezi Mungu.



(6) Tunaamini kwamba giza linapoenea ulimwenguni na wanadamu kuzama kwenye madhambi, zama ambazo bila msaada wa Mungu inawawia shida kujifungua kamba za Shetani, kwa huruma Yake nyingi na Rehema isiyokadirika, Mwenyezi Mungu Huteua kutokana na watumishi Wake wapenzi na watiifu, wale ambao anawapa kazi ya kuuongoza ulimwengu. Mwenyezi Munguanasema katika Quran:



"Na hakuna taifa lolote ila alipita humo Mwonyaji (Sura 35:25).



Ina maana kwamba Mwenyezi Mungu alituma Wajumbe Wakekwa watu wote ulimwenguni. Maisha yao safi na mfano wao mkamilifu ukafanya kazi daima kama mwongozo kwa wanadamu wengine. Wale wanaowapa migongo, wanajishusha. Wale wanaowaelekea wanajipatia radhi ya Mwenyezi Mungu. Wanafunguliwa milango ya baraka Zake. Rehema Yake inawafunika. Wanakuwa waalimu wa kiroho kwa vizazi na vizazi na wanafikia ukuu katika Akhera na dunia. Tunaamini pia kwamba Mitume wa Mwenyezi Mungu ambao toka zamani wamewasaidia wanadamu kuwatoa kwenye giza la madhambi, walikuwa wa daraja mbalimbali za ukuu wa kiroho na walitimiza kwa kadiri mbalimbali makusudio ya kutumwa kwao. Mkuu wa hao wote alikuwa Mtukufu Mtume Muhammad s.a.w. Mwenyezi Mungu alimwita mfalme wa wanadamu naye ni:

"Mjumbekwa wanadamu wote" (34:29).



Mwenyezi Mungu alimfunulia elimu ya mema na mabaya na akambariki kwa msaada Wake. Wafalme wenye nguvu sana ardhini waligwaya kwa kumwogopa. Ardhi yote ikawa mahali pa kuabudia kwa ajili yake (Sahihi Bukhari: mlango wa Tayammum). Wakati ulifika ambao wafuasi wake walionekana dunia nzima; kila sehemu ya dunia kulikuwa waaminio walioinama na kumsujudia Mwenyezi Mungu Mmoja, Mungu asiye kifani. Uadilifu ukaanza kutawala mahala pa batili, huruma mahala pa ukatili. Kama Manabii wa zamani wangeishi wakati wa Mtume s.a.w., wangelazimika kumtii na kumfuata Nabii huyu mkamilifu. Quran Tukufu imesema kweli:



"Na (Kumbukeni) Aliposhika Mwenyezi Mungu ahadi kwa

Manabii: Nikiisha wapeni Kitabu na hekima, kisha awafikieni

Mtume msadikishaji wa yale yaliyo pamoja nanyi, ni juu yenu

kumwamini na kumsaidia" (3:82).



Mtume s.a.w. mwenyewe amesema:



"Lau kama Musa na Isa wangekuwa hai wasingekuwa na njia ila

kunifuata" (Tafsir

Ibn Kathir, Kitabu cha 2, uk. 246).



(7) Tunaamini kwamba Mwenyezi Mungu anasikia maombi ya watumishi Wake wanaomwomba. Anawaondolea shida zao. NiMungu aliye Hai, na Uhai Wake u dhahiri katika mambo yote wakati wote. Mwenyezi Mungu si kama jengo tujengalo tunapochimba kisima ambalo hubomolewa baada ya kuchimbwa kisima. Bali Yeye ni kama nuru na pasipo Yeye hatuoni chochote; ni kama roho ambaye akiondoka kila kitu kitakufa. Akiondolewa Yeye na tuwe mara kama makundi yasiyo na uhai. Sio kweli ya kwamba Mwenyezi Mungu aliumba ulimwengu kishapo akaenda kukaa pembeni. Anaendelea kutoa ukarimu Wake na kufungamana na viumbe Vyake. Wanapojiona wanyonge na wadhaifu, anawageukia kwa msaada Wake. Kama wakimsahau, anawakumbusha juu ya dhati Yake. Ndipo kwa njia ya Mtume Wake anawathibitishia:



"Basi hakika Mimi Nipo karibu. Nayaitikia maombi ya mwombaji

anaponiomba, basi waniitikie na waniamini, ili wapate kuongoka"

(2:187).



Yaani, Mwenyezi Mungu anasikia maombi ya watu Wake. Ni juu yao kumwamini na kumwomba Yeye. Kama wakifanya hivi, bila shaka atawaongoza.



(8) Tunaamini kwamba kwa zama mbalimbali Mwenyezi Mungu hupanga kutokea kwa matukio kwa njia maalum. Matukio ya duniani hayafanyiki kwa kanuni za asili peke yake. Bali, mbali na kanuni hizi kuna kanuni maalumu ambayo kwayo Mwenyezi Mungu hudhihirisha Uwezo Wake, Utukufu Wake na Kudra Yake.Ndiyo Kudra ya Mwenyezi Mungu ambayo baadhi ya watu kwa

ujinga wao wanaikana. Watu kama hao hawaamini chochote ghairi ya kanuni za asili. Naam, kanuni za asili ni za asili tu lakini sio kanuni za Kudra ya Mwenyezi Mungu. Kanuni za Kudra ya Mwenyezi Mungu ni kanuni ambazo kwazo Mwenyezi Mungu huwasaidia wateule Wake, wale anaowapenda; kwa hizo anahilikisha na kufedhehesha maadui wa rafiki Zake. Kama hakungekuwa kanuni hizi, Musa, aliyekuwa dhaifu na mnyonge angewezaje kumshinda Firauni aliyekuwa mfalme jabari na katili? Ingewezekanaje Musa kushinda na Firauni kushindwa ambapo Musa alikuwa dhaifu na Firauni alikuwa mwenye nguvu? Kama hakuna kanuni ghairi ya kanuni za asili, ni kwa vipi Mtukufu Mtume Muhammad s.a.w. angeweza kuishinda Bara Arabu iliyoamua kumwua na kufuta kabisa kazi yake. Katika kila pambano, Mwenyezi Mungu alimsaidia Mtukufu Mtume s.a.w. na kumpa ushindi juu ya maadui zake. Kila shambulio walilofanya maadui liliishia kwa kushindwa kwao, na hatimaye, baada ya miaka kumiya kuuhama mji wa Makka alipokuwa na Sahaba mmoja tu aliyejitoa maisha yake kwa kumlinda Mtume, aliuingia tena mji wa Makka akiwa na Watakatifu elfu kumi. Je, kanuni za asili zinaweza kutoa matukio hayo? Je, zinaweza kuruhusu mambo hayo? Kanuni za asili zinadhamini tu ushindi wa mwenye nguvu dhidi ya dhaifu; na kushindwa kwa dhaifu mbele ya mwenye nguvu.



(9) Tunaamini kwamba mauti sio mwisho wa kuwapo kote kwa wanadamu. Mwanadamu anaishi baada ya mauti na kulipwa matendo yake katika Akhera. Wale watendao matendo mema wanapata malipo ya ukarimu. Wale wanaoasi mafundisho Yake na amri Zake wanakutana na adhabu iliyo ni haki yao. Hakuna kinachoweza kuzuia hesabu hii. Wanadamu lazima waishi na kukutana nayo. Mtu anaweza kuchomwa mpaka akawa majivu na majivu yapeperushwe hewani; anaweza kuliwa na mnyama au ndege au wadudu au ageuke kuwa mavumbi na mavumbi yageuke kitu kingine hata hivyo ataishi tu baada ya mauti na kukutana na Mwumba wake na kutoa maelezo ya matendo yake. Uwezo wa Mwenyezi Mungu unadhamini jambo hili. Sio lazima kwamba mwili

huu uwepo ndipo roho iwe hai. Mwenyezi Mungu anao uwezo wa kuhuisha mwanadamu kutokana na chembe chembe ndogo sana za mwili wake au sehemu nyembamba ya roho yake. Hivi ndivyo itakavyokuwa. Mwili unaweza kugeuka kuwa majivu lakini si lazima yawe si chochote na kutoweka. Hata roho haiwi hivyo bila idhini ya Mwenyezi Mungu.



(10) Tunaamini kwamba makafiri na maadui wa Mwenyezi Mungu, mpaka wasamehewe na Mwenyezi Mungu kwa Rehema Yake kubwa, wataishi mahala paitwapo Jahannamu. Joto kali na baridi kali vitakuwa ndiyo adhabu za mahala hapo, lakini makusudio hayatakuwa kuwaumiza wadhalimu, bali kuwasuluhisha. Huko Motoni, makafiri na maadui wa Mwenyezi Mungu watatumia siku zao kwa mayowe na maombolezo, wakijutia siku walizotumia kwa kufanya maasi. Wataendelea hivi, mpaka Rehema ya Mwenyezi Mungu, ambayo imevizunguka vitu vyote, itakapowazunguka waasi na maasi yao. Hapo ndipo ahadi ya Mwenyezi Mungu iliyotangazwa na Mtukufu Mtume s.a.w. itakapotimia:



"Zama zitaifikia Jahanamu ambapo hamtakuwa yeyote ndani yake; pepo zitavuma na madirisha yatapiga kelele nyingi"

(Tafsir Ma'alim-ut-Tanziil chini ya Aya 107, Sura Hud).



(11) Tumaamini kwamba wale wanaomwamini Mwenyezi Mungu na Mitume Wake, Malaika Wake na Vitabu Vyake; ambao wanafuata, kwa mioyo yao na roho zao, mwongozo utokao Kwake; ambao wanatembea kwa unyenyekevu na wanajinyenyekeza mbeleYake; wale ambao wanaishi kama maskini ijapokuwa wawe matajiri; ambao wanawatumikia wanadamu na kujinyima starehe yao kwa ajili ya wengine; ambao wanaacha kila namna za dhuluma, ukatili na uhaini; ambao ni mifano ya wema kwa wanadamu na kujitenga na tabia mbaya; watu hawa watakwenda mahala paitwapo Jannah. Amani na furaha zitaenea mahala hapo. Hakutakuwa na maumivu. Kila mtu atajipatia furaha na radhi ya Mwenyezi Mungu. Mungu atakuwapo mbele ya wote, fadhili Zake zitamzunguka kila mmoja. Watakuwa karibu sana na Mwenyezi Mungu hivi kwamba kila mmoja atakuwa kama kioo akiangaza kwa Mwenyezi Mungu na sifa Zake kamilifu. Matamanio yote ya ovyo ya mtu yatatoweka. Matamanio ya watu yatakuwa matamanio ya Mwenyezi Mungu. Watakuwa wamefikia uzima wa Milele, kila mmoja akiwa mdhihirishaji wa Mwumba Wake.



Hizi ndizo itikadi zetu. Kama kuna itikadi zingine zozote ambazo mtu lazima awe nazo kabla ya kusemwa kuwa ni Mwislamu, sisi hatuzijui. Maimamu wa Kiislamu hawaelezi itikadi zaidi ya hizi. Tunaamini itikadi zote za Kiislamu na kuzishika kuwa itikadi zetu.



TOFAUTI NA WAISLAMU WENGINE



Sasa, msomaji mpenzi, unaweza kuanza kustaajabu kwa nini tunafikiriwa kuwa tofauti, tunapoamini kwa moyo wote itikadi zote zinazojulikana za Uislamu? Kwa nini Maulamaa wanatutukana? Kwa nini wanatuita makafiri?  Kwa kujibu, ninaweza tu kutaja mambo ambayo kwayo Maulamaa wanasema tumeutoka Uislamu. Mwenyezi Mungu Akulinde na maoni ya kosa na Akufungulie milango ya Rehema Zake!



NABII ISSA ALIKUFA KAMA KAWAIDA



Jambo la kwanza na kubwa kabisa ambalo maadui zetu wanatupinza kwalo ni kwamba sisi tunasadiki kwamba Nabii Isa (a.s.) wa Nazareti alikufa kifo cha asili. Kusadiki kwamba NabiiI sa alikufa kifo cha asili kunasemwa ni kumtusi Nabii Isa, ni kuiacha Quran Tukufu na fundisho la Mtukufu Mtume s.a.w. Ni kweli kuwa tunasadiki kufa kwa Nabii Isa. Lakini si kweli kwamba kusadiki kuwa amekufa ni kumtusi au kuacha Quran Tukufu au kuwa mbali na fundisho la Mtukufu Mtume s.a.w. Mtu akifikiri zaidi juu ya jambo hili mara moja atagunduwa kwamba lawama tunazolaumiwa sisi hazitokani na itikadi yetu juu ya kifo cha Nabii Isa. Bali zinatokana na itikadi yao kwamba Nabii Isa hakufa bali yu mzima mbinguni.

https://c1.staticflickr.com/3/2283/1700703941_3425b68c33.jpg
HADHRAT MIRZA BASHIRUDDIN MAHMOOD AHMAD (RA) Khalifatul Masih II
 Tu Waislamu, na tukiwa Waislamu wajibu wetu wa kwanza ni kuthibitisha Ukuu wa Mwenyezi Mungu na heshima ya Mtukufu Mtume s.a.w. Naam, tunawaamini Manabii wote wa Mwenyezi Mungu. Lakini mapenzi yetu na heshima yetu kwa Mtukufu Mtume s.a.w. ni ya juu sana, kwa sababu yeye alijitolea kwa ajili yetu; alijikaribishia mauti kwa kutuokoa na kifo cha kiroho; alihuzunika sana kwa ajili yetu. Aliacha starehe yake kwa ajili yetu. Alijishusha
ili sisi tusimame juu. Alipanga namna za manufaa yetu na kutuombea starehe za daima. Aliacha miguu yake ivimbe kwa kusimama ibadani. Akiwa mtakatifu, aliomba tutibiwe madhambi yetu, kutuokoa katika Moto; alisali mpaka msala ukaloa kwa machozi. Alilia mpaka kifua chake kilitoa sauti kama birika la

maji yanayochemka. Kwa ajili yetu alisogeza Huruma ya Mwenyezi Mungu;

alitaabika kwa kumpendeza Yeye na kutusaidia sisi pia. Alitufanya tufunikwe na shuka ya Rehema Yake, kawa la Huruma Yake. Alijitahidi na akapata njia ambazo kwazo tuweze kumridhisha Mwenyezi Mungu; njia ambazo kwazo tuweze pia kuungana naye. Aliyoyafanya kwa ajili yetu hayajapata kufanywa kabla na Nabii yeyote kwa ajili ya kaumu yake. Basi, fatwa za ukafiri zinatupendeza sisi. Tungependa kuitwa makafiri kuliko kumfahamu Nabii Isa kuwa sawa na Mungu Mwumba wetu, Mruzuku wetu na Mlinzi wetu, ambaye anatupa mkate wetu wa kila siku na elimu na mwongozo tunaotegemea kwa

starehe yetu ya kiroho. Fatwa za ukafiri zinakaribishwa mno nasi kuliko kusadiki kwamba Nabii Isa yuko hai mbinguni bila ya kula wala kunywa. Tunamheshimu Nabii Isa. Lakini kwa nini? Kwa sababu ni Nabii wa Mungu wetu. Twampenda Masihi. Lakini kwa nini? Kwa sababu Mungu alimpenda naye alimpenda Mungu. Kumheshimu kwetu ni kwa sababu ya kumheshimu Mwenyezi Mungu. Tunawezaje kumweka juu ya Mwenyezi Mungu na kumdharau Mungu kwa sababu yake? Je, tuwape nguvu wahubiri wa Kikristo ambao kazi yao kila siku ni kutafuta makosa katika Uislamu na Quran Tukufu? Je, tuwafanye wafikiri kwamba Nabii Isa alikuwa Mungu? Kwani, kama hakuwa Mungu, anawezaje kuwa hai mbinguni? Tunawezaje kwa vinywa vyetu wenyewe, kusema jambo livunjalo heshima ya Umoja wa Mwenyezi Mungu? Tunawezaje kuiharibu na kuangamiza dini Yake? Maulamaa wako huru kufanya watakalo; wanaweza kuwachochea watu dhidi yetu, watupige mawe au watuue. Hatuwezi kumwacha Mwenyezi Mungu kwa ajili ya Nabii Isa. Tungekubali mauti kama tungelazimishwa kusema kwamba Nabii Isa yuko hai mbinguni kama Mungu – Nabii Isa ambaye Wakristo wanaamini kuwa ni mwana wa Mungu na ambaye kwa ajili yake wanautupa Umoja na Kujitegemea kwa Mwenyezi Mungu. Laiti tungebakia ujingani, ingelikuwa vingine.

Lakini tangu macho yetu yafumbuliwe na Mtume wa Mwenyezi Mungu, ambaye ametuonesha Umoja wa Mwenyezi Mungu, na Utukufu Wake, na Uwezo Wake, na Ukuu Wake na ukarimu Wake hatuwezi kufanya hivyo. Na litokee lolote, hatuwezi kumwacha Mwenyezi Mungu kwa sababu ya kiumbe mwanadamu. Kama tufanye hivi, hatujui tutakuwa wapi. Heshima ni ya Mwenyezi Mungu na vyeo vyote vinatoka Kwake. Tunapoona waziwazi kwa kusadiki kuwa Nabii Isa yuko mbinguni ni kumtusi Mwenyezi Mungu, hatuwezi kusema ya kuwa itikadi hii ni kweli. Sisi hatuwezi kuelewa kwa nini kusadiki kifo cha Nabii Isa ni kumtusi Isa. Mitume wakubwa wakubwa kuliko Nabii Isa wamekufa na vifo vyao havikuleta fedheha kwa ajili yao. Vilevile kifo cha Isa hakiwezi Kuwa fedheha kwake. Lakini kama, kudhania yasiyowezekana, tukutanishwe na mawili - Mungu au Isa - na kama tutakiwe kufanya uchaguzi, bila shaka tutamchagua Mwenyezi Mungu. Tuna hakika kuwa Nabii Isa mwenyewe, ambaye alimpenda sana Mwenyezi Mungu, asingekubali kamwe cheo kinachomheshimisha Isa na kumdharaulisha Mwenyezi Mungu na Umoja Wake. Quran Tukufu inatufundisha hivihivi:



"Masihi hatebeua kuwa mtumishi wa Mwenyezi Mungu wala

Malaika waliokurubishwa" (4:173).



                       QURAN NA HADITHI VINASEMA NABII ISA KAFA

Tunafungwa hapa na Neno la Mwenyezi Mungu. Tunaposoma katika Quran Tukufu:



"Na nilikuwa shahidi juu yao nilipokuwa kati yao, lakini

Uliponifisha Wewe Ukawa Mchungaji juu yao, na Wewe ni Shahidi

juu ya kila kitu" (5:118).



Mwenyezi Mungu katika jina la Nabii Isa anatangaza kwamba Wakristo walipotea baada ya kifo cha Isa. Alipokuwa hai, walishika imani safi. Kwa kusoma haya ndani Ya Quran, tunawezaje kufikiri kuwa Isa si mfu bali yu mzima mbinguni? Pia tunasoma ndani ya Quran Tukufu:



"Ewe Isa, kwa yakini Mimi Nitakufisha na Nitakuinua Kwangu,

na Nitakutakasa na (masingizio ya) wale waliokufuru, na

Nitawaweka wale waliokufuata juu ya wale waliokufuru mpaka

siku ya Kiyama" (3:56).



Nabii Isa aliinuliwa kwa Mwenyezi Mungu baada ya kifo chake. Maneno "Nitakuinua" au "Nitakunyanyua" yanakuja baada ya maneno "Nitakufisha". Ni lazima tufuate kanuni za lugha. Linalotajwa mwanzo, lazima litendeke kwanza. Lakini pengine Maulamaa wanajua kanuni hizi vizuri zaidi kuliko Mwenyezi Mungu. Huenda wanafikiri kuwa ijapokuwa "Nitakuinua" imetajwa mwisho katika aya hii, lakini ingetajwa mwanzo. Lakini Mwenyezi Mungu ni Mwenye hekima kinyume na maarifa yetu. Anajua vizuri mno namna gani mawazo yanatakiwa yaelezwe. Katika usemi Wake hakuwezi kuwa na kosa, wala kupotoka neno moja katika mpango wa maneno Yake. Ni Mwumba wetu nasi ni viumbe Vyake.

Tutathubutuje kuona kosa katika usemi Wake? Lakini Maulamaa wanaonekana kufikiri kwamba kunaweza kuwa na kosa katika usemi wa Mwenyezi Mungu na sio katika wao kuelewa usemi huo. Sisi hatuwezi kusema hivi; kwani, tunaona ni maangamio matupu fikara hii. Hali tuna macho, hatuwezi kutumbukia shimoni. Hali tunajua, hatuwezi kunywa kikombe cha sumu. Baada ya Mwenyezi Mungu, tunampenda Mtukufu Mtume Muhammad s.a.w. tu. Ni Mkuu wa Manabii wote. Hakuna mwanadamu mwingine, awe nabii au la, ambaye amefanya hata sehemu ndogo sana ya yale aliyoyafanya Mtukufu Mtume s.a.w. kwa ajili yetu. Hatuwezi kumheshimu zaidi mtu mwingine. Haiwezekani kwetu kufikiri kwamba Isa, Masihi, yu hai mbinguni hali Muhammad, Mtume wetu Mtukufu, amezikwa chini ya ardhi. Hatuwezi kufikiri hivyo. Tunasadiki kwamba kwa daraja ya kiroho, Mtukufu Mtume s.a.w. amesimama juu sana kuliko Isa. Inawezekana kweli Mwenyezi Mungu ampandishe Isa mbinguni kwa sababu ya alama ndogo sana ya hatari kwa maisha yake, lakini asimpandishe Mtukufu Mtume s.a.w. walau karibu ya nyota alipokuwa akifukuzwa na maadui zake huku na huko? Hatuwezi kusadiki kwamba bwana wetu yu mfu ardhini lakini Isa yu hai mbinguni. Tunaona kifo ni afadhali kuliko imani hii ambayo ni fedheha mbele ya Wakristo. Lakini, mshukuru Mwenyezi Mungu, mambo hayako hivyo. Mwenyezi Mungu hangeweza, na kwa kweli, hajapata kumfanyia Mtukufu Mtume s.a.w. namna kama hii. Mwenyezi Mungu Ndiye Bwana wa mahakimu wote. Yeye Mwenyewe alimwita Mtukufu Mtume s.a.w. kama Mfalme wa wanadamu, hangeweza kumjali zaidi Isa. Kwa ajili ya Mtukufu Mtume s.a.w. Mwenyezi Mungu aliutikisa ulimwengu wote. Yeyote aliyefikiri kumfedhehesha, alifedheheka mwenyewe. Je, angeweza kumfedhehi Mtukufu Mtume s.a.w. na kuwapa maadui nafasi ya kuchekelea fedheha yake? Kufikiri kuwa Mtukufu Mtume s.a.w. yu mfu ardhini na Isa wa Nazareti yu hai mbinguni, kunanisisimua nywele. Ninaona ni kiroja na fedheha pia, kwa hiyo ninajiona nikitangaza "La, Mungu hawezi kufanya hivi". Anampenda Mtukufu Mtume s.a.w. kuliko yeyote mwingine. Hangeweza kumwacha afe na kuzikwa lakini ampandishe Isa mbinguni. Laiti mtu yeyote angestahiki kuwa hai na kupanda
https://bilaltahir20.files.wordpress.com/2015/04/hazrat-mirza-tahir-ahmad-sahib.jpg
HADHRAT MIRZA TAHIR AHMAD (RA), Khalifatul Masih IV
mbinguni huyo angekuwa Mtukufu Mtume s.a.w. Kama amekufa kama kawaida, basi Manabii wengine wamekufa kama kawaida. Hali ya kujua cheo kikubwa sana alichonacho Mtukufu Mtume s.a.w. mbele ya Mwenyezi Mungu, hatuwezi hata kidogo kufikiri kwamba angefanyiwa na Mungu Mwenyezi duni ya yale aliyofanyiwa Isa. Hatuwezi kufikiri kwamba zama za Hijra, Mtukufu Mtume s.a.w. alipojificha ndani ya pango la Thaur, ambalo ili alifikie ilimbidi abebwe na Seyidna Abubakar r.a., Mwenyezi Mungu hakupeleka Malaika wowote kumwokoa; lakini Mayahudi walipotaka kumkamata Isa, Mungu akamnyanyua mpaka mbingu ya nne ili kumwokoa na mpango wa Mayahudi wa kumwua. Katika vita ya Uhud, Mtukufu Mtume s.a.w. alibakiwa na Waislamu wachache tu waliomzunguka alipokuwa akishambuliwa na maadui. Mungu hakupeleka Malaika wowote, wala hakuumba pale zingaombwe ili maadui walishambulie badala ya kumshambulia Mtukufu Mtume s.a.w., na kuvunja meno ya zingaombwe hilo badala ya meno ya Mtukufu Mtume s.a.w. Mwenyezi Mungu aliwaacha maadui wamshambulie Mtukufu Mtume s.a.w. mwenyewe na mpaka alipoanguka kama aliyekufa, maadui wakapiga kelele za shangwe na hoihoi kwamba (Mungu apishe mbali). wamemwua Muhammad, Mtume wa Mungu. Lakini kwa kumhusu Isa, Mungu hakuacha hata maumivu kidogo tu yamsumbue. Mara tu Mayahudi walipoamua kumkamata, Mungu akamnyanyua mbinguni, na mahala pake, wakamkamata mmoja wa maadui zake ambaye Mungu alimfanya awe na sura ya Isa, na hivyo wakamwamba msalabani huyu badala ya kumwamba Isa! Tunastaajabu juu ya matokeo ya watu hawa. Upande mmoja wanadai kumpenda sana Mtukufu Mtume s.a.w.; na upande mwingine, wenyewe wanaelekea kumdhararu na kumfedhehesha. Na hawakomei hapo. Wanaendelea mbele na kutoa Fatwa za ukafiri kwa wale ambao kwa sababu ya kumpenda Mtume s.a.w. wanakataa kushiriki kwenye zile itikadi zinazomweka mtu mwingine juu ya Mtukufu Mtume s.a.w. Tunashangaa wana muradi gani kwa ukafiri? Je, kufikiri kuwa Mtukufu Mtume s.a.w. ana daraja ya juu zaidi ya Manabii wengine na kumtolea heshima inayomstahiki ni ukafiri? Kama huu ni ukafiri, basi Wallahi ukafiri wetu una thamani mara nyingi zaidi kuliko imani ya wale wanaotupa ukafiri huo. Seyidna Mirza Ghulam Ahmad, Masihi Aliyeahidiwa, alisema sawa:



"Baada ya Mwenyezi Mungu, nimelevywa na mapenzi ya

Muhammad. Kama hii ni kufuru, Wallahi, mimi ndiye kafiri

mkubwa wa makafiri wote".



Ni lazima sote tufe siku moja na kusimama mbele ya Mwenyezi Mungu na kujibu tutakayoulizwa. Kwa nini tumwogope mwanadamu yeyote? Wanadamu wanaweza kutupa dhara gani? Tunamwogopa Mwenyezi Mungu tu na tunampenda Yeye tu. Baada Yake, tunampenda na kumheshimu Mtukufu Mtume s.a.w. zaidi. Kama kwa ajili ya Mtukufu Mtume s.a.w. italazimu kutoa heshima yetu, manufaa na vitu vya dunia hii, tutaona rahisi sana. Lakini kumdharau Mtukufu Mtume s.a.w. hatuwezi kuvumilia hata kidogo. Hali ya kujua utakatifu aliokuwa nao, elimu ya kiroho aliyokuwa nayo na ukaribu aliokuwa nao na Mwenyezi Mungu hatuwezi kufikiri kwamba Mwenyezi Mungu alimpenda mtu mwingine yeyote zaidi kuliko alivyompenda Mtukufu Mtume s.a.w. Kama sisi tuchukue fikara hii, tutastahiki adhabu zaidi kuliko wengine wote. Tunajua vizuri sana kwamba waliomkataa Mtukufu Mtume s.a.w. walimwambia wakimtaka aoneshe mwujiza wa kupanda mbinguni.

Walisema:



"Au upande mbinguni; na hatutaamini kupanda kwako mpaka

ututeremshie kitabu tukisome" (17:94).



Kwa kujibu ombi lao hili, Mwenyezi Mungu hakumpa Mtume s.a.w. uwezo wa kuonesha mwujiza aliotakiwa kuuonesha. Badalayake, Mwenyezi Mungu alimwambia Mtukufu Mtume s.a.w.:



Sema: Mola wangu ni Mtakatifu! mimi siye ila ni mtu tu, Mtume"

(17:94).



Lakini, Maulamaa wanavyofundisha, Nabii Isa, MwenyeziMungu alimpandisha mbinguni. Mtukufu Mtume s.a.w. anapoombwa kupanda mbinguni, kupanda mbinguni kunasemwa na Mwenyezi Mungu kuwa hakuwezekani na mwanadamu. Lakini Isa anapandishwa mbinguni bila haja hata kidogo. Kama hili ni kweli, je, haitakuwa kwamba Isa hakuwa mwanadamu bali Mungu? Mungu atulinde na mawazo haya. Je, haitaleta maana kwamba Isa alikuwa na daraja ya juu zaidi na alipendwa na Mungu zaidi kuliko Mtukufu Mtume s.a.w.? Lakini tunajua, na ni dhahiri kama jua, kwamba Mtukufu Mtume s.a.w. ni m'bora na mkuu wa manabii wote. Hali ya kujua hivi, tunawezaje kufikiri kwamba Mtukufu Mtume s.a.w. hakupanda mbinguni, bali alikufa na kuzikwa ardhini kama kawaida, lakini Isa apae mbinguni na kuwa huko hai kwa miaka mamia na mamia? Sio tu kwamba ni jambo la ghera juu Ya Mtume s.a.w. Bali ni jambo la ukweli wake pia, ukweli wa madai yake. Je, hakusema Mtume s.a.w. kwamba:



"Lau kama Musa na Isa wangalikuwa hai,

wasingekuwa na njia ila kunifuata?" (Zurqani, Kitabu cha 6 uk. 54).



Kama Isa yu hai, basi madai haya ya Mtukufu Mtume s.a.w. ni lazima yasemwe kuwa ni ya uongo. Maneno ya Mtukufu Mtume s.a.w. yana maana sana na yako dhahiri. Anasema, "Lau kama" Musa na Isa wangalikuwa hai. Hii "Lau kama" inawaweka Musa na Isa pamoja na ina maana kwamba hawa wawili ni wafu. Musa si mzima wala Isa si hai. Hili ni tangazo la maana sana la Mtukufu Mtume s.a.w. Baada ya kusikia tangazo hili, hakuna mfuasi wa kweli wa Mtukufu Mtume s.a.w. anayeweza kufikiri kwamba Isa yu hai mbinguni. Maana kama Isa yu hai mbinguni, tangazo la Mtukufu Mtume s.a.w. linageuka kuwa la uwongo; pia elimu yake juu ya jambo lenyewe. Kuna tamko jingine la maana sana la Mtukufu Mtume s.a.w. Wakati wa ugonjwa wake wa mwisho, alimwambia binti yake Fatima:



"Hakika Jibrili alikuwa akinisomea Quran mara moja kila mwaka.

Na mwaka huu amenisomea mara mbili. Na akaniambia kuwa kila

Nabii aliishi nusu ya umri wa Nabii aliyemtangulia. Akaniambia

pia ya kuwa Isa bin Mariamu aliishi miaka 120. Kwa hiyo, nafikiri

ninaweza kuishi mpaka miaka 60" (Mawaahib-ul-ladunniyyah, kilichoandikwa na Qastalani, Kitabu cha I uk. 42).



Tamko hili ni la ufunuo. Mtukufu Mtume s.a.w. hakusema lolote kwa kujikinai, bali alieleza aliyoambiwa na Jibrili, Malaika wa Wahyi. Sehemu ya maana sana ya tamko hili ni kwamba Isa aliishi miaka 120. Kwa maelezo ya Agano Jipya, Isa alikuwa yapata miaka 32 au 33 hivi alipowambwa msalabani na "akapaa mbinguni." Kama Isa kweli "alipaa" basi umri wake mpaka wakati wa Mtukufu Mtume s.a.w. unakuwa karibu miaka 600, sio 120. Kama aliyoyapokea Mtukufu Mtume s.a.w. kutoka kwa Jibrili ni ya kweli, Mtume s.a.w. kuwa mfuasi wa Musa aliyewahuisha wafuasi wa Musa. Silsila ya Musa ilidumu mpaka muda aliopenda Mwenyezi Mungu. Hatimaye ulipofika wakati wa kukoma kwa silsila hiyo, Mwenyezi Mungu aliwaachia wafuasi wa Musa na kuelekea dhuria wa Ismail kuinua Nabii kwa ajili ya kuwaongoza wanadamu. Kama sasa, aje Nabii wa silsila ya Musa kuwaongoza wafuasi wa Mtukufu Mtume s.a.w., itakuwa na maana (Mungu apishe mbali) kwamba Mwenyezi Mungu ameamua kuikomesha silsila ya Mtukufu Mtume s.a.w. kama alivyokomesha silsila ya Musa, na ya kwamba mahala pake anaanzisha silsila mpya. Itakuwa na maana (Mungu apishe mbali tena) ya kwamba nguvu ya kiroho ya Mtume Mtukufu s.a.w. haina athari tena hivi kwamba inashindwa kumpatia hata mfuasi mmoja nuru iliyo muhimu kwa kuhuishia na kuongozea wafuasi wake tokana na mafundisho na mfano wake. Ole wao! juu ya kosa dogo sana linalotaka kushusha hadhi yao wenyewe hawawezi kuvumilia; hawakubali dosari yoyote au upungufu ndani yao. Lakini hawachelei kuingiza dosari na udhaifu kwa Mtukufu Mtume s.a.w., na bado wanadai kuwa wapenzi wa Mtume s.a.w. Mtukufu. Yana faida gani mapenzi ya kubwata kwa midomo tu lakini hayapatikani moyoni? Imani isiyofuatana na vitendo ina maana gani? Kama Waislamu walimpenda kweli Mtukufu Mtume s.a.w. wasingechekelea kufika kwa Nabii wa Kiyahudi kuja kuhuisha wafuasi wa Mtukufu Mtume s.a.w. Ni nani anayeomba kwa jirani yake haja anayoweza kuikidhi nyumbani mwake mwenyewe? Ni nani anayemwomba msaada mwenzake ambapo anaweza kujisaidia mwenyewe? Masheikh wanaofikiri na kufundisha wafuasi wa Mtume s.a.w. kwamba Masihi wa Nazaretiatafika mara ya pili wakati wa haja, wenyewe wanapita kiasi katika kulinda uluwa wao hivikwamba katika majadiliano ya dini wangependa kuanguka kuliko kukubali msaada kwa mwingine yeyote. Kama kuna msaada wowote, hawawi na furaha: wanaumwa na kusema: "Je, tumeishiwa elimu sisi hivi kwamba tuhitaji msaada wa wengine?" Lakini inapofika kwa Mtukufu Mtume s.a.w. wanakuwa wepesi mara moja! Wanakuwa chapu sana kuamini na kufundisha ya kuwa zama wafuasi wa Mtukufu Mtume s.a.w. wanapohitaji kuhuishwa, hawatapata uhuishaji huo kutokana na wafuasi wa Mtukufu Mtume s.a.w. mwenyewe, sio kutokana na mvuto wa kiroho wa mwenyewe Mtume s.a.w., bali kutokana na ukarimu wa Nabii wa silsila ya zamani, ambaye hakupata chochote katika mafundisho ya Mtume s.a.w. Je, watu wamekuwa wafu na masugu kiasi hiki? Je, wamepotewa na uwezo wote wa kufikiri na kuhisi? Wanahifadhi heshima yao na uluwa wao wenyewe, lakini siyo kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na Mtume s.a.w. Wanaweza kuonesha ghadhabu na makasiriko kwa maadui zao binafsi, lakini siyo kwa wale wanaomkosea Mungu na Mtume Wake? Tunaulizwa kwa nini tunakataa kufika mara ya pili kwa Nabii wa Kiisraeli. Lakini tunaweza tufanyeje? Hatuwezi kubadili mioyo yetu. Hatuwezi kuonesha mahaba yetu kwa Mtukufu Mtume s.a.w. isipokuwa katika njia za kiasili. Heshima ya Mtukufu Mtume s.a.w. ni penzi mno kwetu. Hatuwezi kufikiri kwamba kwa ajili ya kuhuisha wafuasi wake, Mtume s.a.w. ahitaji msaada wa Nabii aliye mbali na yeye na kuwa mdeni wake. Hatuwezi kufikiri hata kidogo kwamba siku ya Kiyama, wanadamu tokea wa mwanzo mpaka wa mwisho kabisa watakapokusanyika mbele ya Mwenyezi Mungu, na matendo na mafanikio yao yote yatatangazwa, Mtume s.a.w. atasimama na mzigo wa deni la Masihi Mwisraeli, Malaika wakitangaza mbele ya wanadamu wote ya kwamba wafuasi wa Mtukufu Mtume s.a.w. walipopotea, mfano wa kiroho wa Mtukufu huyu mwenyewe ulishindwa kuwahuisha kwenye nguvu ya kiroho, kwa kumhurumia Mtukufu Mtume s.a.w., Masihi wa Kiisraeli akajitupa kutoka peponi na kurudi ulimwenguni kuwahuisha. Hatuwezi kuingiza fikara kama hii. Tungependa ndimi zetu zikatwe kuliko kumkashifu Mtume s.a.w. kwa udhalilifu namna hii. Tungependa mikono yetu ife ganzi kabisa kuliko kuandika jambo la namna hii kwa Mtukufu Mtume s.a.w. Mtukufu Mtume s.a.w. ni mpenzi wa Mwenyezi Mungu. Nguvu yake ya kiroho haiwezi kamwe kufutika. Yu Muhuri wa Manabii. Fadhili na baraka zake za kiroho hazimaliziki kabisa. Hana haja kupata deni kwa Manabii wengine wowote na kudaiwa nao. Manabii wengine ndio wanaodaiwa naye. Hakuna Nabii hata mmoja ambaye Mtukufu Mtume s.a.w. hakutangaza ukweli wake mbele ya waliomkataa. Yalikuwa mafundisho ya Mtukufu Mtume s.a.w. yaliyowaingiza mamilioni ya wanadamu katika imani juu ya Manabii ambao walikuwa hawana habari nao. Kuna Waislamu milioni 80 katika India (Wakati makala. Wachache miongoni mwao walitoka nchi za nje. Wengine ni wazawa hasa wa nchi hii na walikuwa hawajapata kusikia juu ya Nabii yeyote yule. Lakini tangu walipomwamini Mtukufu Mtume Muhammad, walianza kumwamini Ibrahimu, Musa, Isa na wengine (amani ya Mungu iwe juu yao). 
Kama wasingelikuwa Waislamu, wangeendelea kuwadharau Manabii hawa, hata kuwatukana pia. wangeendelea kuwafahamu kuwa walikuwa waongo kama vile Wahindu katika India wanavyoendelea kuamini hivyo mpaka leo. Kadhalika Afghanistan, China na Iran. Wenyeji wa nchi hizi hawakuwa na habari, hivyo hawakumkubali Musa na Isa kuwa Manabii. Ujumbe wa Mtume s.a.w. ukaenea katika Wakati kitabu hiki kilipoandikwa nchi hizi, na watu wake wakamwamini Mtume s.a.w. na kila alichofundisha. Walianza kuwajua Manabii wengine na kuwaheshimu kama Manabii wa kweli. Hivyo Mtukufu Mtume s.a.w. amewatwika mzigo wa deni Manabii waliomtangulia wote. Ukweli wao ulikuwa haujulikani, Mtukufu Mtume s.a.w. akaujulisha kwa watu. Mtukufu Mtume s.a.w. hana deni la mtu yeyote. Fadhili na baraka za mafundisho yake lazima ziendelee milele. Kwa ajili ya kuhuisha wafuasi wake hana haja ya msaada wa Nabii mwingine. Wakati wowote haja ya namna hii inapotokea, Mwenyezi Mungu atainua mmoja wa wafuasi wake (Mtume s.a.w.) awaongoze wafuasi wengine na kutengeneza kilichoharibika. Huyo atapata kila kitu kutoka kwa Mtukufu Mtume s.a.w. Atajifunza kila kitu kutoka kwake. Chochote awezacho kufanya, katika kuhuisha na kujenga upya, kitakuwa ni cha Mtukufu Mtume s.a.w. mwenyewe. Chochote apatacho mwanafunzi kutoka kwa mwalimu, hakika ni cha mwalimu. Mfuasi hawezi kutengwa mbali na Imam wake, na hivihivi mwanafunzi hawezi kutengwa mbali na mwalimu wake. Mfuasi anayewaongoza wafuasi wenzake atawiwa na Mtukufu Mtume s.a.w. na moyo wake na ubongo wake utakuwa umejaa mapenzi yake. Kwa ufupi, kuja kwa Nabii wa zamani kwa ajili ya kuhuishawafuasi wa Mtukufu Mtume s.a.w. ni matusi kwa Mtukufu Mtume s.a.w.. Tukio kama hili linaweza kudhuru ukuu wa Mtukufu Mtume s.a.w. Kadhalika litakadhibisha fundisho la Quran Tukufu lisemalo:



"Hakika Mwenyezi Mungu Habadili yaliyoko kwa watu mpaka

wabadili yaliyomo nafsini mwao" (13:12)



Hali ya kuona fundisho hili la Quran, hatuna budi kukubali ama ya kuwa Mtukufu Mtume s.a.w. (Mungu apishe mbali), amekuwa hastahiki ahadi ya Mwenyezi Mungu kwa kubadilika hali yake, auya kwamba Mwenyezi Mungu mwenyewe amekhalifu ahadi yake. Kwa wengine wote, mwendo wa Mwenyezi Mungu haukuwa kunyang'anya zawadi aliyokwisha itoa; lakini kwa Mtukufu Mtume s.a.w. afanye vingine! Kuingiza fikira kama hii kunafanya ukafiri. Kunafanya ama kumkataa Mwenyezi Mungu au kumkataa Mtume s.a.w. Kwa sababu ya matokeo haya ya hatari tumechoka na itikadi kama hizi. Tunaamini kwamba Masihi, ambaye kufika kwake kulitabiriwa na Mtukufu Mtume s.a.w. ni wa kutokana na wafuasi wa Mtukufu Mtume s.a.w. Mwenyezi Mungu ana hiyari kumpa cheo hiki mtu yeyote.



MASIHI NA MAHDI NI MTU MMOJA



Katika Hadithi za Mtukufu Mtume s.a.w. inadhihirika pia ya kwamba Masihi Aliyeahidiwa ilikuwa awe ni mfuasi wa Mtukufu Mtume s.a.w. Hadithi moja inatuambia kuwa:



"Mahdi siye ila ni Isa". (Ibni Majah - Kitabul Fitan, Baab Shiddatuz-zaman)



Hadithi nyingine inasema:



Mtakuwaje atakapowafikieni mwana wa Mariam na kiongozi wenu atakuwa miongoni mwenu?" (Bukhari, Kitabul-Anbiya, mlango Nuzuul Isa bin Maryam).



Hadithi hizi mbili zinatoa shaka kabisa kwamba Masihi mwenyewe atakuwa Mahdi. Atawaongoza wafuasi wa Mtukufu Mtume s.a.w. atatokana miongoni mwao, hatakuwa mtu wa nje. Kufikiri kuwa Masihi na Mahdi ni watu wawili mbalimbali ni kosa. Ni kinyume na Ishara ya wazi iliyomo ndani ya Hadithi:



                                            "Mahdi siye ila ni Isa."



 Inafaa waaminio wema kufikiri kwa makini matamshi ya Bwana wao. Kama matamshi haya yanaonekana yanahitilafiana, ni juu yetu kujaribu kuondoa hitilafu hiyo. Kama Mtukufu Mtume s.a.w. alisema upande mmoja, kwamba Mahdi atadhihiri kabla ya Masihi, na kisha Masihi atajiunga na Mahdi na kumfuata katika ibada; na upande mwingine, kwamba Masihi mwenyewe ndiye Mahdi, tutafanyaje? Je, tukubali tamko moja na kukataa jingine? Au je, siyo wajibu wetu kwamba tufikirie matamshi haya mawili kwa makini sana na kujaribu kupatanisha moja na jingine? Matamshi mawili haya yanaweza kupatana kama tulitumie moja kulitafsiri jingine. Inaonekana ya kwamba ahadi ya kudhihiri kwa Mahdi ilibebwa ndani ya maneno yaliyodhanisha kwamba Masihi na Mahdi ni watu wawili mbalimbali. Maoni haya yanasahihishwa na Hadithi isemayo kwamba "Mahdi siye ila ni Isa". Hadithi hii inabainisha ya kuwa hiyo Hadithi nyingine ni ya methali. Ina maana kwamba mfuasi wa Mtukufu Mtume s.a.w. atatokea kwa ajili ya kuuhuisha ulimwengu, lakini hatakuwa na cheo cha Nabii. Halafu ile ahadi ya kufika mara ya pili kwa Nabii Isa itatimia katika nafsi yake na atajitangaza kuwa Masihi Aliyeahidiwa. Kwa hiyo, Hadithiinatuambia ya kuwa Masihi Aliyeahidiwa ataanzia na kazi ya Mujaddid wa Kiislamu ambaye atakuja pewa kazi ya Masihi. Vyeo viwili vitafuatana kwa mtu huyohuyo mmoja. Bishara za kiungu mara nyingi hutumia methali. Ni mara chache sana zinapotumia vingine.


https://www.alislam.org/images/khalifa1.gif
HADHRAT MAULVI NURUDDIN (RA), kHALIFATUL MASIH I


Kama tafsiri yetu ya Hadithi hizi si sahihi, basi kumebakia njia mbili tu kwa ajili ya atafutaye ukweli: nazo zote ni za upuuzi na za hatari pia. Ama, tukubali ya kuwa ile Hadithi inayoeleza kuwa Masihi na Mahdi ni mtu mmoja siyo Hadithi ya kweli, au, tukubali ya kuwa Masihi na Mahdi ni watu wawili mbalimbali na ya kwamba dhamiri ya Hadithi ni kuashiria hitilafu ya fadhila ya kiroho ya watu wawili hao. Inaweza kuwa na maana ya kwamba Mahdi wa kweli atakuwa Masihi. Maana nyingine, ni kwamba Mahdi atakuwa duni ya Masihi. Itakuwa kama kusema: "Hakuna mwanachuoni ila fulani." Tusemapo hivyo, hatuna maana hasa kwamba hakuna mwingine ajuaye. Bali tuna maana kwamba huyu fulani anajua sana. Kwa vyovyote tafsiri hizi mbili ni za hatari. Moja inatutaka tuifanye kuwa ni ya uwongo Hadithi ya Mtukufu Mtume s.a.w. iliyo ya kweli kwa kila mizani. Nyingine inafahamisha kuwa Mahdi atakuwa si chochote mbele ya Masihi. Fikara hii itakuwa kinyume na Hadithi zinazofundisha ya kuwa Mahdi atakuwa Imam na Masihi atakuwa mfuasi anayesimama nyuma ya Imam katika sala ya jamaa. Hivyo njia zote mbili ni za kipuuzi. Tafsiri zilizo bora ambazo tunaweza kuzitolea Hadithi hizi ni hizi tu ya kuwa zinatabiri kuja kwa Mjumbe toka miongoni mwa wafuasi wa Mtukufu Mtume s.a.w. Mjumbe huyu kwanza atadhihiri akiwa Mujaddid na baadaye atajitangaza kuwa Masihi wa bishara. Mtu huyo huyo atakuwa Mahdi na Masihi pia. Hakutakuwa na tafsiri yenye maana ya Hadithi hizi isipokuwa tafsiri hii.

            NUZUUL SIO MAANA YAKE KUSHUKA KUTOKA MBINGUNI

Sababu ya mgogoro huu ni kwamba kila mtu amepotezwa na neno nuzuul lililomo ndani ya Hadithi. Maana yake halisi ni kushuka. Kwa hiyo watu wengi wamepotezwa na fikara kwamba kwa vile Masihi imesemwa atashuka ni budi awe yule Masihi wa kwanza. Sasa basi, ni kosa kufikiri ya kwamba neno nuzuul siku zote lina maana ya kushuka kutoka juu. Neno nuzuul linaashiria tu ni ubora ulioje wa kitu kinachosemwa kuwa kitashuka. Linatuambia kuwa kitu hicho cha kushuka kitakuwa chombo cha utukufu na uwezo wa Mwenyezi Mungu. Vitu kama hivi vinasemwa kuwa huwashukia wanadamu kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Hii maana ya kushuka ni sawa na matumizi ya neno hili ndani ya Quran Tukufu mahala pengi inasema:



"Kisha Mwenyezi Mungu Akateremsha utulivu Wake juu ya Mtume Wake" (9:26).



"Kisha baada ya huzuni Aliwateremshieni utulivu - usingizi ambao

ulifunika kundi moja katika ninyi" (3:155).



"Na Akawateremshieni wanyama wanne kwa jozi" (39:7).



"Hakika Tumekuteremshieni nguo zifichazo aibu zenu na

mapambo; na nguo za utawa ndizo bora. Hayo ni katika Ishara za

Mwenyezi Mungu ili wapate kushika mauidha" (7:27).



"Na Tukawateremshieni Manna na Salwa" (2:58).



"Na tukakiteremsha chuma, chenye nguvu nyingi na manufaa kwa

watu; na ili Mwenyezi Mungu Ajulishe anayemsaidia Yeye na

Mitume wake kwa siri. Kwa yakini Mwenyezi Mungu ni Hodari,

Mwenye nguvu" (57:26).



"Na kama Mwenyezi Mungu Angetoa riziki nyingi kwa watumishi

wake bila shaka wangaliasi ardhini, lakini Huiteremsha kwa

kipimo akipendacho. Hakika Yeye kwa watumishi Wake ni

Mwenye habari, Mwenye kuona" (42:28).



Kila mtu anajua ya kuwa utulivu ni sifa ya akili ya mwanadamu na usingizi ni kazi ya ubongo wake. Wanyama, nguo, mashamba, salwa, chuma na vitu vingine vinakuwa ardhini au baadhi vinatoka ndani ya ardhi. Havishuki au kudondoka kutoka mbinguni. Wala kushuka kwao kutoka mbinguni sio maelezo yaliyotumiwa na Quran Tukufu. Maelezo ya Quran Tukufu yako wazi kabisa. Inasema:



"Na Akaweka humo milima juu ya uso wake, na Akabarikia humo

na Akapima humo chakula chake katika nyakati nne, ni sawa kwa waulizao" (41:11).



Katika aya hii, Mwenyezi Mungu anaashiria kwamba maumbile yote ya kiasili na kuumbwa kwa mali za namna mbalimbali kunahitaji elimu ya namna nyingi ili kufahamike. Elimu hii Mwenyezi Mungu Huifunua sehemu sehemu. Sehemu imekwisha funuliwa, na sehemu itafunuliwa wakati ujao. Kila swali jipya litatolewa na yote yatapata majibu yake. Lakini, anasema Mwenyezi Mungu tumeeleza kuumbwa kwa maumbile ya kiasili na kuumbwa kwa mali ya asili kwa njia ambayo watu wa nyakati zote (sawa na uwezo wao) watapata ndani yake maelezo ya kweli na ya kutosheleza.



Hivyo, kutokana na Quran Tukufu, inadhihirika kwamba vitu vyote vya kiasili hutoka kwa Mwenyezi Mungu - vinatolewa na Mwenyezi Mungu - na tena havidondoki kutoka mbinguni.