JavaScriptSDK

Tuesday, May 31, 2016

TAIFA HALIWEZI KUIMARIKA PASIPO VIJANA KUWA IMARA!



Khuddam-ul Ahmadiyya ni Tanzimu au Tawi la Vijana wa Kiislamu wa Jumuiya ya Waislamu Wa-Ahmadiyya Duniani. Tanzimu au Tawi hili ni la vijana wa Kiahmadiyya kuanzia miaka 15 mpaka 40. Khuddam-ul Ahmadiyya ilianzishwa rasmi na Khalifatul Masih II, Hadhrat Mirza Bashiruddin Mahmood Ahmad (ra) mwaka 1938. Kulingana na Khalifatul Masih II, maneno Khuddamul Ahmadiyya maana yake vijana waliopo katika kundi hili ni Watumishi wa Ahmadiyya. Katika hotuba yake yenye kukumbukwa sana aliyoitoa Aprili 1, 1938,  katika msikiti wa Al Aqsa uliopo Qadian, India, Khalifatul Masih II (ra):
http://www.amjinternational.org/wp-content/themes/striking/cache/images/KM2-212x300-212x300.jpg
Khalifatul Masih II(ra), Mwanzilishi wa Majlis Khuddamul Ahmadiyya
“Nimekuwa nikisisitiza jumuiya kuhusiana na ukweli kwamba, Kuimarika kwa Taifa Lolote Hakuwezi Kutimia Pasipo Vijana Wake Kuwa Imara.Jumuiya yetu haiwezi kupata maenedeleo ya kweli mpaka pale vizazi vipya havijatekeleza Ujumbe na Mafundisho sahihi Kiislamu ambayo Mtume S.A.W aliyaleta Duniani. Khuddamul Ahmadiyya maana yake ni Watumishi wa Ahmadiyya. Jina hili daima litaendelea kuwakumbusha kwamba wao ni watumishi, na si kutumikiwa. Mnatakiwa  mdhihirishe na muimarishe vipawa vyenu kwamna iliyo bora. Ikiwa mtaonesha mfano mwema kwa wengine, itakuwa rahisi kuwavutia kujiunga na jumuiya yenu.”

https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/9/98/Khuddam-ul-Ahmadiyya_1-2.svg/2000px-Khuddam-ul-Ahmadiyya_1-2.svg.png
Bendera rasmi ya Majlis Khuddamul Ahmadiyya ambayo inatumiwa na vijana wa Ki-Ahmadiyya kuanzia miaka 15 hadi 40
Majlis Khuddamul Ahmadiyya Tanzania ni sehemu ya kauli hiyo ya Khalifatul Masih II (ra) kwani madhumuni ya kuanzishwa kwake yanabeba maana nzima ya Utumishi si kwa Jumuiya pekee bali utumishi kwa viumbe vyote vya Allah kwa lengo la kupata radhi yake.

ITAENDELEA…

No comments: